Je, Vyuo vya Afya vya Serikali Vina Uzuri Huo?
Vyuo vya afyavya serikali vimegawanyika katika makundi 2 makubwa. Vyuo vya kati na vya elimu ya juu.
Kama ulikuwa unahitaji kufahamu orodha ya vyuo vya afya vya serikali vilivyopo karibu yako, hapa tutakupatia PdF ya bure. Pia, nitakuonesha namna unaweza kuvifahamu vyuo vyote unapotumia AFYAColleges App.
🔗 Soma pia: Vyuo vya Afya Tanzania (Orodha Kamili na Tofauti Zake)
Orodha Vyuo vya afya vya kati vya serikali
Vyuo vya kati vya serikali hutoa mafunzo katika ngazi ya diploma / stashahada na astashahada (certificate). Hii ni orodha ya vyuo vya afya vya kati vya serikali katika baadhi ya mikoa. Unaweza kufahamu orodha kamili kwenye AfyaColleges App.
| Jina la Chuo | Mkoa | Aina ya Chuo |
| KCMC Assistant Medical Officers Training | Kilimanjaro | Serikali |
| Mtwara COTC | Mtwara | Serikali |
| Mwanza Centre (Lyamungo) | Mwanza | Serikali |
| Singida Medical Training Centre | Singida | Serikali |
| Tanga Centre (Bumbuli) | Tanga | Serikali |
| Mbeya Medical Training Centre | Mbeya | Serikali |
Usibahatishe Mustakabali Wako!
Kuchagua chuo sahihi ni hatua ya kwanza kuelekea kuwa daktari au nesi mwenye mafanikio. Fahamu vigezo muhimu vya kuzingatia ili usipoteze muda na gharama kwenye chuo kisichokidhi viwango.
FAHAMU JINSI YA KUCHAGUA CHUO BORA⭐ Mwongozo huu umewasaidia zaidi ya wanafunzi 1,000 mwaka huu.
Orodha Ya Vyuo vya Elimu ya Juu vya Serikali
Vyuo vya juu vya serikali hutoa mafunzo katika ngazi ya shahada (degree), uzamili (masters) na Uzamivu (PhD). Hii ni orodha ya vyuo vya afya vya juu vya serikali katika baadhi ya mikoa. Unaweza kufahamu orodha kamili kwenye AfyaColleges App.
| Jina la Chuo | Mkoa | Kozi Zitolewazo (Shahada/Degree) |
| MUHAS (Muhimbili University of Health and Allied Sciences) | Dar es Salaam | Medicine (MD), Pharmacy, Nursing, Dentistry, Laboratory Sciences, Environmental Health, Physiotherapy, Radiotherapy. |
| UDOM (University of Dodoma) | Dodoma | Medicine (MD), Nursing, Medical Laboratory Sciences, Health Information Management. |
| MUST (Mbeya University of Science and Technology) | Mbeya | Biomedical Engineering, Medical Laboratory Sciences. |
| SUA (Sokoine University of Agriculture) | Morogoro | Veterinary Medicine, Biotechnology and Laboratory Sciences. |
| Mzumbe University | Morogoro | Health Systems Management. |
| OUT (Open University of Tanzania) | Nchi Nzima | Public Health, Nursing. |
| DIT (Dar es Salaam Institute of Technology) | Dar es Salaam | Bachelor of Engineering in Biomedical Engineering. |
| MoCU (Moshi Co-operative University) | Kilimanjaro | Health Administration. |
Gharama za vyuo vya afya vya serikali
Gharama ya vyuo vya afya ya serikali huanzia hutegemea ngazi ya elimu na kozi husika. Kwa kozi za diploma ada huwa kati ya TSh. 700,000/= mpaka 1,400,000/=.
Ada ya kozi za afya za elimu ya juu huanzi TSh. 1,500,000/= mpaka 2,500,000/= kwa mwaka. Kumbuka hizi ni ada (tuition fee), hazijumuishi pesa zote mwanafunzi anazohitaji ili kuishi vyuoni.